KUTOKA MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA NCHINI: KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI TANZANIA AFUNGA RASMI MAFUNZO YA ULINZI WA AMANI KWA MAAFISA MAGEREZA TOKA NCHI ZA SADC, MKOANI KILIMANJARO
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akikabidhi
cheti kwa Mmoja wa Washiriki wa Mafunzo ya Ulinzi wa Amani, Mkaguzi
Msaidizi wa Magereza Nchini Tanzania, Pendo Kazumba. Mafunzo hayo
yamefanyika kwa wiki mbili na yameendeshwa na Kituo cha Mafunzo cha SADC
kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza Tanzania(kushoto) ni Mkuu wa
Kituo cha Mafunzo cha SADC Bregedia Jenerali Christopher Chellah.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja
akitoa hotuba fupi ya ufungaji wa Mafunzo ya Ulinzi wa Amani ambayo
yamefanyika kwa wiki mbili katika Chuo cha Maafisa Uhamiaji, Moshi
Mkoani Kilimanjaro ambapo jumla ya Maafisa Magereza 27 toka Nchi za SADC
ikiwemo Tanzania, Botswana, Afrika Kusini, Mauritius, Swaziland na
Zimbabwe wameshiriki kikamilifu Mafunzo hayo.
Wakufunzi wa Mafunzo hayo wakisikiliza hotuba fupi ya ufungaji wa
Mafunzo ya Ulinzi wa Amani kwa Maafisa Magereza toka Nchi za SADC. Jumla
ya Wahitimu 27 toka Nchi za SADC wameshiriki Mafunzo hayo kikamilifu
katika Chuo cha Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro(wa kwanza kulia) ni
Mratibu wa Mafunzo hayo, Kanali Sambulo Ndlovu toka Zimbabwe(wa pili
kulia) ni Mkufunzi toka Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Charles
Novart(wa tatu kushoto) ni Mkufunzi toka Tanzania, Ahmad Mwidadi(wa
pili kulia) ni Mkufunzi toka Zambia, Mrakibu wa Polisi Nchini Zambia,
Edward Njovu.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja
akifanya mahojiano Maalum na Waandishi wa Habari toka Vyombo vya TBC1 na
ITV Mkoani Kilimanjaro mara tu baada ya kufunga rasmi Mafunzo ya Ulinzi
wa Amani kwa Maafisa Magereza toka Nchi za SADC leo Oktoba 2, 2014 Chuo
cha Maafisa Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja
akifanya mahojiano Maalum na Waandishi wa Habari toka Vyombo vya TBC1 na
ITV Mkoani Kilimanjaro mara tu baada ya kufunga rasmi Mafunzo ya Ulinzi
wa Amani kwa Maafisa Magereza toka Nchi za SADC leo Oktoba 2, 2014 Chuo
cha Maafisa Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini Tanzania, John Casmir
Minja(wa sita kushoto) na Mkuu wa Kituo cha Mafunzo cha SADC, Bregedia
Jenerali Christopher Chellah(wa tano kulia) wakiwa katika picha ya
pamoja na Maafisa Magereza Wanawake toka Nchi za SADC ambao wameshiriki
kikamilifu Mafunzo ya wiki mbili ya Ulinzi wa Amani katika Chuo cha
Maafisa Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro.
Mkuu wa Kituo cha Mafunzo cha SADC, Bregedia Jenerali Christopher
Chellah(kushoto) akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini
Tanzania, John Casmir Minja(kulia) mara tu baada ya kufunga rasmi
Mafunzo ya Ulinzi wa Amani kwa Maafisa Magereza toka Nchi za
SADC(katikati) ni Mmoja wa Washiriki wa Mafunzo hayo toka Nchini
Tanzania, Mkaguzi Msaidizi wa Magereza, Pendo Kazumba.
Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(katikati) akiwa katika
picha ya pamoja na Maafisa Magereza toka Nchi za SADC(waliosimama)
walioshiriki Mafunzo ya Ulinzi wa Amani ambayo yamefanyika kwa wiki
mbili katika Chuo cha Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro. Mafunzo hayo
yamefungwa leo na Kamishna Jenerali wa Magereza ambapo jumla ya Maafisa
Magereza 27 toka Nchi za SADC ikiwemo Tanzania, Mauritius, Afrika
Kusini, Swaziland, Botswana, Namibian na Zimbabwe wamehitimu Mafunzo
hayo Maalum ya Ulinzi wa Amani.Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la
Magereza
No comments: