KIKUNDI CHA VIJANA WAJIITAO PANYA ROAD WAFUNGA MITAA NA KUZUA TAFRANI KUBWA JIJINI DAR
Kamanda
wa Polisi Kanda Maalum jijini Dar,Kamanda Kova akitoa ufafanuzi wa
habari za taharuki katika vyombo vya habari hususani
televisheni,kuhusiana na sakata la kundi la Vijana wajiitao Panya
Road,amesema suala hilo lilikuwa dogo,lakini baadhi ya watu wamelikuza
na kupelekea hofu kubwa kwa Wananchi ''Jiji mpaka sasa liko salama na
wananchi watulie wasiwe na hofu kwa sababu jeshi la Polisi liko imara
kuhakikisha amani inakuwepo ya kutosha,na hao vijana hawawezi kulishinda
Jeshi la Polisi'',alisema.Alisema Wananchi waondoe hofu waendelee na
shughuli zao kama kawaida.
katika
hali isiyo ya Kawaida na ya kuogopesha,kumeibuka taharuki kubwa usiku
huu kwa Wakazi wa maeneo mbalimabali ya jiji la
Dar,ikiwemo,Sinza,Kinondoni,Mwananyamala,Mabibo,Magomeni,Manzese,Kagera
na Mburahati kwa kile kinachoelezwa kuwa vijana waitwao Panya Road
wamevamia maeneo hayo na kuwajeruhi watu kwa vitu vyenye ncha kali,visu
na mapanga na kuwapora vitu (mali zao) walivyokuwa navyo,kama vile
haitoshi baadhi yao wamevunjiwa vioo vya magari yao.
Chanzo
chetu cha habari kimeeleza kuwa vijana hao waitwao Panya Road wameibuka
na kufanya uhalifu huo mara baada ya tukio la Mwenzao mmoja kudaiwa
kuuwawa na Polisi.
Aidha
Chanzo hicho kimebainisha kuwa baada ya taarifa kusambaa kwa
haraka,kimeeleza kuwa Jeshi la Polisi limeingia kazini kuwasaka
watuhumiwa hao walioibua tafrani kubwa usiku huu.
Wadau tutazidi kuwaletea taarifa zaidi kuhusiana na tukio hilo kadiri ya zitakavyokuwa zikipatikana.
No comments: