Makabiliano makali yametokea kati ya waasi wa kishia wa Houthi na vikosi vya usalama katika ikulu ya Rais ambao inasadikiwa waasi hao wameiteka ikulu ya Rais
Walioshuhudia makabiliano hayo wanasema waasi hao walipambana na vikosi vya usalama kwa muda kabla ya kuingia katika ikulu ya Rais.
Awali,
Rais Abd Rabbuh Mansour Hadi alifanya mazungumzo ya dharura na washauri
wake siku moja baada ya vifo vya watu tisa kufuatia makabiliano mengine
kati ya waasi hao na wanajeshi mnamo Jumatatu.
Makubaliano yalifikiwa lakini waasi wa Houthis waliendelea kuzingira ikulu ya Rais na makao ya waziri mkuu.
Kiongozi
wa waasi hao anatarajiwa kutoa hotuba baadaye leo wakati baraza la
usalama la Umoja wa Mataifa likijiandaa kwa mkutano wa dharura kujadili
hali nchini Yemen.
Kanali Saleh al-Jamalani, ambaye ni mkuu wa
kikosi cha ulinzi wa ikulu ya Rais Abed Rabbo Mansour Hadi, ameambia
sjirika la habari la AP kwamba waasi haowalivamia ikulu nyakti za
mchana.
Rais Hadi inaarufiwa hakuwa katika makao hayo wakati waasi walioivamia ikulu
Habari Kutoka BBCswahil.com
Habari Kutoka BBCswahil.com
No comments: