Polisi katika Jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo, wamefyatua risasi hewani ili kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wamekusanyika katika mji mkuu Kinshasa kupinga sheria mpya ya uchaguzi
Serikali inasema kuwa watu wanne walifariki katika vurugu za Jumatatu
ingawa upinzani unasema idadi huo huenda ikwa kujuu kuliko
iliyonakiliwa.
Wanafunzi wameweka vizuizi barabarani na pia
wameshuhjudiwa wakichoma magurudumu, katika barabara zinazoelekea katika
chuo kikuu mjini humo.
Wanatuhumu wanasia wanaomuunga mkono Rais
Joseph Kabila ambaye muhulka wake wa pili unatarajiwa kumalizika mwaka
ujao kwa kujaribu kujiongeza muda mamlakani kwa kuidhinisha mipango ya
kufanyika sensa ambayo itachelewesha uchaguzi kwa miaka mingi.
Vurugu hizi zinashuhudiwa huku baraza la Senate likidadisi mswada ambao huenda ukasababisha Rais Kabila kuongezwa muda mamlakani
Vijana walioandamana kwa vurugugu, waliteketeza magurudumu ya magari, kupora maduka na kurusha mawe.
Wanafunzi waliambia BBC kuwa polisi walivamia chuo chao baada ya wao kuanza kuandamana.
Walisema polisi walingia katika vyumba vyao na kuwafyatulia gesi ya kutoa machozi.
Viongozi
wa upinzani walitoa wito kwa waandamanaji kwenda barabarani kupinga
mipango ya serikali kumuongeza muda zaidi mamlakani Rais Joseph Kabila
huku wakiutaja mpango huo kuwa mapinduzi ya kikatiba.
Mswada huo unapendekeza kufanytika sensa kote nchini ambayo itachukua kipindi cha miaka mitatu.
Rais Kabila amekuwa mamlakani tangu mwaka 2001.
Muhula wake wa pili unakamilika mwaka 2016 kikatiba
No comments: