NAIBU WAZIRI WA FEDHA MWIGULU NCHEMBA AADHIMISHA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUTEMBELEA YATIMA, WAGONJWA NA KUCHANGIA DAMU
Naibu
Waziri wa Fedha,Mwigulu Mchemba leo ameadhimisha miaka 40 tangu
kuzaliwa kwake. Katika maadhimisho hayo Naibu waziri huyo ambaye pia ni
Mbunge wa Iramba Magharibi ameitumia siku hiyo ya jana kwa kutembelea
wagonjwa katika wodi ya Wazazi ya Hospitali ya Mwananyamala, Dar es
Salaam, kuchangia damu pamoja na kuwatembelea na kuwapa zawadi yatima
katika kituo cha CHAKUWAMA.
Mwigulu akiwa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala.
Mwigulu Mchemba akiangalia mmoja wa watoto waliozaliwa siku ya leo.
Naibu Waziri Mwigulu Mchemba akichangia damu katika benki ya damu Salama.
Akipiga
picha ya pamoja na watumishi wa Benki ya Damu Salama. Father Kidevu
Blog inaungana na wananchi wa jimbo la Iramba Magharibu, Familia yake na
watanzania wote kwa ujumla kumtakia heri na fanaka katika maisha yake
na Mungu amjalie Hekima na Busara.
No comments: