Timu ya Simba Sc imeibuka kidedea kwa kutwaa kombe la mapinduzi kwa mikwaju 4-3 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo ulipigwa kwenye dimba la Amaani Visiwani Zanzibar
Dakika tisini za mchezo za kawaida zilimalizika kwa timu hizi kwenda
sululu ya bila kufungana ndipo changamoto ya mikwaju ya penati ikafuata .
Penati
za simba zilifugwa na Awadh Juma, Hassan Kessy, Hassan Isihaka na Dan
Ssenrukuma wakati ya Shaaban Kisiga iliokolewa na Kipa Said Mohamed.
Penati
za Mtibwa Sugar zilifungwa na Ally Lundenga, Shaaban Nditi na Ramadhan
Kichuya huku Ibrahim Rajab ikigonga mwamba huku penati ya Vincent
Barnabas ikiokolewa na kipa Ivo Mapunda.
Nahodha wa Simba, Hassan
Isihaka,alikabidhiwa Kombe la Mapinduzi pamoja na Shilingi Milioni 10
kutoka kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta
Ali Mohammed Shein.
Kipa Said Mohammed wa Mtibwa Sugar amekuwa
kipa bora wa michuano,beki wa kati wa Mtibwa Sugar, Salim Mbonde
ameibuka kuwa mchezaji bora wa michuano.Mfungaji bora amekuwa Simon
Msuva wa Yanga ambaye alifunga mabao manne.
No comments: