Umoja wa mataifa imezituhumu serikali za Tanzania na Burundi kuhusiana na hali katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
Ripoti mpya ya kundi la wataalamu wa umoja huo kuhusu Congo,
imeituhumu Tanzania kwa kuwaruhusu viongozi wa kundi la waasi wa FDLR
kuandaa mikutano nchini humo.
Imeeleza pia kwamba wanajeshi wa Burundi wametekeleza unyanyasaji wa kingono.
Taarifa
hiyo ya Umoja wa mataifa inasema kuwa tangu mwaka wa 2013, viongozi wa
FDLR na baadhi ya washirika wao wa kisiasa kutoka Ulaya wamekuwa
wakikutana nchini Tanzania
Lakini wachunguzi wa Umoja wa mataifa walipoiuliza serikali ya
Tanzania kujibu madai haya ilikanusha kabisa kuwahi kuakaribisha
mikutano yoyote ya waasi ndani ya ardhi yake na kuongeza kuwa hakujawahi
kuwa na mazungumzo yoyote kati ya majeshi yake na wapiganaji wa FDLR.
Umoja
wamataifa umesema pia kuwa una ushahidi wa pesa zilizotumwa kutoka
taifa hilo la Afrika Mashariki kwa baadhi ya washukiwa nchini Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo.
Ripoti hiyo pia imelaumu kundi hilo la
FDLR kwa kutotekeleza ahadi yao ya kusalimisha silaha na kujisalimisha
kufikia Januari mwaka huu.
UN inasema kuwa FDLR wamewatuma wazee
waliodhoofika kiafya pekee kujisalimisha na kukabidhi silaha chache sana
ambazo zina hitilafu.
Kundi la FDLR, liliundwa mwaka wa 2000 na
wahutu waliokimbilia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia mauaji ya
kimbari ya Rwanda
Kundi hilo linapinga utawala wa kitutsi na ushawishi wake katika eneo la maziwa makuu.
Rwanda
imekuwa ikitazama kundi hilo kama tisho kubwa kwa utawala uliopo na kwa
kauli moja na Umoja wa mataifa imekuwa ikishinikiza kupokonywa silaha
kwa wapiganaji wake.
Ripoti hiyo pia imetoa madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kimapenzi unaofanywa na wanajeshi wa Burundi katika Kivu ya Kusini.
Wataalamu
hao wa Umoja wa mataifa wamependekeza serikali za Burundi na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo zifanyie uchunguzi madai hayo ambayo wanasisitiza
yalifanywa namajeshiya Burundi pamoja na kikundi cha vijana wapiganaji
wajulikanao kama Imbonerakure.
No comments: