SERIKALI IMEAGIZA WAKANDARASI WOTE WALIOSITISHA UJENZI KUANZA KAZI MARA MOJA.
Serikali imeagiza wakandarasi wote waliositisha ujenzi wa miundombinu
mbalimbali nchini kuanza kazi mara moja baada ya kufanikiwa kuwalipa
madeni yao zaidi ya shillingi billion 400 kati ya deni la trilion 1.2
lililoachwa na serikali ya awamu ya nne.
Agizo hilo limetolewa na waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano
Prof, Makame Mbarawa mkoani Morogoro ambapo amesema katika kipindi cha
miezi mitatu serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kuwalipa wakandarasi
kiasi cha shiling bilion 400 ambapo mpaka kufikia mwezi juni mwaka huu
wakandarasi wote watakuwa wamelipwa fedha zao, huku agizo hilo likienda
sambamba na kumtaka mkandarasi wa barabara ya Dakawa, Turiani kuendelea
na ujenzi wa barabara.
Aidha katika hatua nyingine waziri Mbarawa akiwa katika ziara yake
mkoani Morogoro akiambatana na naibu wazi wake Mhandisi Edwin Ngonyani
wametembelea katika karakana ya TRL ambako inafanyika na kuzungumza na
wafanyakazi ambapo alikuwa mbogo kwa kuwaonya wale wote watakao bainika
kutengeneza ajali za treni kwa makudi serikali haitawavumilia,
watafukuzwa kazi sambamba na kufikishwa mahakani.
Nao wafanyakazi wa shirika hilo wamotoa malalamiko yao kwa waziri
huyo wakidai serikali kuwasahau kwa kuimarisha miundo mbinu ikiwa ni
pamoja na stahiki zao na kusababisha kuishi maisha ya kiumaskini.
Waziri Mbarawa katika ziara yake yakukagua miradi mbalimbali
alitembelea barabara ya Magole Turiani, kitio cha mawasiliano cha
Halotel, karakana ya reli pamoja na kituo cha mizani cha Mikese mkoani
Morogoro.
No comments: