Ads Top

WAZIRI MKUU: KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA BANDARI KUZIBA UKWEPAJI KODI KUPITIA UINGIZAJI MAFUTA

  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mhandisi, Aloys Mtei (kulia) kuhusu  mabomba yanayotawanya mafuta kwenda kwenye matangi makubwa ya makampuni mbalimbali kwenye eneo la Kigambo jini Dar es salaam Februari 11, 2016.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyeshwa na kamimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamla ya bandari Tanzania, Mhandisi Aloys Mtei eneo zinakotia nanga meli kubwa zinazoleta mafuta nchini kupitia bandari ya Dar es salaam Februari 11, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua eneo lenye mabomba yanayotumika kupitisha mafuta kutoka kwenye meli  kupitia bandari ya Dar es slaam wkatia lipofanya ziara ya kukagua miundombinu yenye mianya ya ukwepaji kodi hasa kwenye mafuta yanayoingia nchini Februari 11, 2016. 

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa Flow Meter eneo la Kigamboni jijini Dar es salaam Februari 11, 2016. Mtambo huo utatumika kupima wingi wamafuta yanayotoka kwenye meli na kuingizwa hapa nchini. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymound Mushi. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Ujezi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (kulia) wikimsikiliza Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Bandari Tanzania,Mhandisi, Aloys Mtei wakati alipotoa maelezo kuhusu uingizaji wa mafuta kutoka nje ya nchi kupitia bandari ya Dar es salaam Februari 11, 2016.Mheshimiwa majaliwa alikuwa katika ziara ya kukagua miundombinu yenye mianya ya ukwepaji kodi kwenye mafuta yanayoingia nchini kupitia bandadari hiyo.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua eneo ambalo mafuta hufunguliwa na kufungwa ili kwenda kwenye matangi ya kuhifadhia mafuta ya makampuni mbalimbali yanayoagiza mafuta toka nje ya nchi wakati alipokwenda enero la Kigamboni jijini Dar es salaam kuonamianya inayotumika kukwepa kodi za mafuta yanayoagizwa nje ya nchikupitia bandari ya Dar es salaamFebruari 11, 2016. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitaka maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo na Mizani, Bibi Magdalena Chuwa (kulia) kuhusu sababu zilizomfanya azuie matumizi ya flow Meter katika kuhakiki kiwango cha mafuta yanayoingia nchini kupitia bandari ya Dar es salaam wakati alipofanya ziara kwenye badari hiyo Februari11, 2016. katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Raymound Mushi.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.