WAZIRI WA UJENZI PROF. MBARAWA AWAONYA WATUMISHI WA TTCL WASIO WAAMINIFU MWANZA.
Prof. Mbarawa ametoa onyo hilo baada ya kutembelea na kujionea
hatua za ujenzi wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa awamu ya tatu
katika vituo vya Ghana na Mwanza telephone house eneo la posta jijini
Mwanza.
Meneja wa TTCL mkoa wa Mwanza Johnbosco Kalisa kilio chake ni madeni ya wateja sugu zikiwemo idara za serikali.
Baadhi ya wafanyakazi wa TTCL na posta mkoani Mwanza wanaeleza
kilio chao kwa waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Mh. Prof.
Makame Mbarawa juu ya changamoto wanazokumbana nazo katika utendaji wao
wa kazi za siku kwa siku.
Pamoja na TTCL kupewa jukumu la kuongoza mkongo wa taifa kwa
kutumia teknolojia ya Optical Fibre, ambapo Mwanza ni kiungo kikuu cha
kanda ya ziwa na nchi jirani, ulinzi na usalama wa mkongo huo bado
unakabiliwa na hujuma zinazodaiwa kufanywa kwa makusudi na baadhi ya
watu pamoja na wakandarasi wa barabara wanapokuwa kazini.
No comments: