Ads Top

VIGOGO WANNE WA MSD WASIMAMISHWA KAZI KWA UBADHILIFU WA SHILINGI BILIONI 1.5.


Serikali imewasimamisha kazi vigogo wanne wa bohari kuu ya dawa MSD kwa tuhuma za ubadhilifu wa shilingi bilioni moja na nusu kwa kukiuka taratibu za manunuzi.

Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Mh Ummy Mwalimu amewataja maafisa hao waliosimamishwa kuwa ni mkurugenzi wa kanda huduma za wateja Cosmas Mwaifwan, mkurugenzi wa fedha Joseph Tesha, mkurugenzi wa ugavi Misanga Muja na Henry Mchunga, mkurugenzi wa manunuzi.

Mh Mwalimu ametoa taarifa hiyo alipokuwa akipokea vitanda zaidi ya 100 kutoka MSD zoezi lililoambatana na kuvifunga katika wodi mpya ikiwa ni utekelezaji wa agizo la rais John Magufuli alipotembelea wodi ya wazazi hivi karibuni na kukuta wakiwa wamelala chini.


Katibu mkuu wa wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Mpoki Ulisubisya akizungumza wakati wa ufungaji wa vitanda hivyo amesema jengo hilo lina uwezo wa kulaza kina mama 120 na kuhusu watumishi wa wizara yake waliokuwa wanatumia jengo hilo amesema.
Baadhi ya kina mama ambao walikuwa wanakabiliwa na kero ya kulala chini na ambao wamepata nafasi ya kuhamia jengo jipya mbali na kumshukuru rais Magufuli wamesema.

Wakati huohuo Mh Ummy ametangaza mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu kuwa umerudi tena jijini Dar es Salaam ambapo wagonjwa sita kutoka wilaya ya Temeke wamegunduliwa huku mikoa 11 ikiripotiwa kuwa na wagonjwa wapya na mkoa wa Iringa ukiongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa ambao ni 199.
chanzo ITV

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.