MKANDARASI AKAMATWA NA POLISI KWA KUSHINDWA KULIPA VIBARUA WILAYANI UKEREWE.
Mkandarasi wa kampuni ya Nyakarungu CIVIL CONSTRUCTION, Harrison Odila ametiwa nguvuni na jeshi la polisi mjini Nansio wilayani Ukerewe kwa madai ya kushindwa kuwalipa vibarua zaidi ya 100 waliokuwa wanajenga barabara ya Butiriti – Guguyu yenye urefu wa kilometa tano kwa kiwango cha udongo.
Mkandarasi huyo amekamatwa na askari polisi wa kituo cha Nansio
akiwa katika ofisi za makao makuu ya halmashauri ya wilaya ya Ukerewe,
saa chache baada ya vibarua hao kufanya maandamano ya kudai malipo yao
kiasi cha shilingi milioni moja laki mbili na elfu hamsini.
Diwani wa kata ya ngoma ambako barabara hiyo imejengwa na
kukamilika tangu mwezi Septemba Mwaka jana Bw.Msingi Musese amelalamikia
kitendo kilichofanywa na mkandarasi huyo cha kuwapiga danadana vibarua
hao.
Mkuu wa idara ya ujenzi katika halmashauri ya wilaya ya Ukerewe
mhandisi mapinduzi Magesa Mwita ambaye ameshuhudia mkandarasi wa kampuni
hiyo ya nyakarungu akitiwa nguvuni na askari polisi wawili alikuwa na
haya ya kusema kuhusiana na wakandarasi wenye tabia kama hiyo.
Haya ndiyo majibu ya mkandarasi huyo,Harrison Odila katika
mahojiano na ITV baada ya kukutana na vibarua hao ofisi za halmashauri
ya wilaya ya Ukerewe.
chanzo ITV
No comments: