Ads Top

RAIS DKT.MAGUFULI AMESEMA KUWA HATOINGILIA MGOGORO WA UCHAGUZI ZANZIBAR.

Rais Dakta.John Pombe Magufuli amesema hataingilia mgogoroo wa Zanzibar na kuwataka wenye malalamiko waende mahakamani.

Akiongea na wazeee wa mkoa wa Dar es Salaam rais Magufuli amesema  katiba ya Zanzibar imeweka uhuru wa tume ya uchaguzi kama ilivyo tume ya uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano na hivyo kama kiongozi anayeheshimu utawala wa sheria hawezi kuingilia suala hilo.

Dakta.Magufuli ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuongea na wazee wa Dar es Salam tangu kuingia madarakani ameomba watanzania kuiunga mkono serikali ya awamu ya tano katika kudhibiti wabadhirifu  ili kuelekeza fedha zitakazopatikana kwenye mipango ya maedneleo nakuapa kutovumilia wala rushwa na wazembe huku akionya wanaokejeli kuwa kasii yake ni nguvu ya soda.

Kuhusu michango rais amesema katika elimu michango yote ni hiari na kwamba wakuu wa mikoa  na wilaya watapimwa kwa kadiri wanavyotekeleza wajibu wao  kwa kutatua kero za wananchi ikiwemo kero ya madawati.

Rais hakuacha kusisitiza watanzania wazalendo kutumia fursa ya serikali ya awamu ya tano kuwekeza  katika nchi yao kwa kadiri wanavyoweza.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.