Ads Top

WAKAZI WA KIJIJI CHA LASHAINI MONDULI WALALA NJE BAADA YA KUBOMOLEWA NYUMBA ZAO

Baadhi ya wakazi  wa kijiji cha Lashaini wilaya ya Monduli Mkoani Arusha hawana mahali pa kuishi  na wamelazimika  kulala nje baada ya nyumba zao kubomolewa kwa madai ya kujenga katika eneo linalodaiwa kuwa ni la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWT).
  
Wakizungumza na ITV iliyo fika katika eneo hilo na kujionea hali halisi  huku baadhi ya watoto na wanawake wakiwa wameketi katika vitanda vilivyo njee baada ya nyumba kubomolewa na kudai kuwa wapo kwenye maeneo halali na waliiomba  serikali ipeleke kipimo cha GPS kama ilivyo ahidi mwaka jana ili kuhakiki maeneo hayo lakini hadi sasa haijapeleka watalam na kwamba wakigundulika wapo ndani ya eneo la jeshi wapo tayari kuondoka  lakini hada sasa wanaimani awajavuka nje ya maeneo yao halali.

Afisa ardhi wa wilaya ya Monduli Abili Mwanga amesema kimsingi wananchi wamejenga nje ya eneo linalo milikiwa na jeshi na kwamba  wamebolewa kimakosa na hata litakapo pimwa kwa bado eneo hilo litakuwa nje ya eneo linalodaiwa.

Akizungumza baada ya kutembelea nyumba zilizo bomolewa mkuu wa wilaya ya Monduli Francis Miti amesema amezungumza na viongozi  wa jeshi na kumpa maelezo kwanini wamevunja nyumba hizo lakini mazungumzo ya kina yatafanyika juma tatu ili kupata ufumbuzi wa mgogoro huo kabla ya kuleta madhara zaidi.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.