Ads Top

VIGOGO WA TRL WAFIKISHWA KATIKA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU JIJINI DSM.

 
Aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa shirika la reli Tanzania (TRL), Kipallo Kisamfu na wenzake 10 wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashiataka tisa yakiwemo ya matumizi mabaya ya madaraka kwa kupitisha ununuzi wa mabehewa mabovu 25.


Watuhumiwa hao pia kwa mujibu wa hati ya mashitaka wanadaiwa kupitisha malipo ya zaidi ya shilingi bilioni 2.8 kinyume na taratibu. 

Washtakiwa hao walisomewa mashitaka yao mbele ya hakimu mkazi mwandamizi, Emmilius Mchauru. Huku upande wa jamhuri uoliongozwa na mawakili wa serikali waandamizi, Shadrack Kimaro, Theophil Mutakyawa na waendesha mashitaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru), Max Ally na Maghela Ndimbo.

Max alidai katika shitaka la kwanza, kati ya februari mosi, 2013 na juni 30, 2014 makao makuu ya TRL, mshtakiwa Kisamfu akiwa mkurugenzi mtendaji kwa nia ovu alitumia vibaya nafasi yake kwa kushindwa kusimamia zabuni na kusababisha kampuni ya M/S Hindusthan Engineering and Industries Limited kupata faida.

Shitaka la pili linamkabili mshtakiwa wa sita, Mafikiri, ambaye ilidaiwa kuwa kati ya julai mosi na agosti 31, mwaka 2013, makao makuu ya TRL, akiwa fundi mkuu, alitumia vibaya madaraka yake kwa kupitisha ramani ya mabehewa iliyoandaliwa kinyume cha sheria na kuisababishia kampuni ya  m/s hindusthan engineering and industries limited kupata faida.

Max aliendelea kudai kuwa kati ya januari mosi na februari 28, mwaka 2014 makao makuu ya TRL, akiwa kaimu mkuu wa ufundi, aliidhinisha kampuni ya M/S Hindusthan Engineering and Industries Limited kufanya ukarabati wa mabehewa 25 bila kujiridhisha na maombi ya tenda hiyo.

Katika shitaka jingine, ilidaiwa kuwa kati ya januari mosi na februari 28, mwaka 2013, TRL, mshtakiwa wa nne, saba, nane, tisa na 10, wakiwa wajumbe wa kamati ya kutathmini zabuni walitumia madaraka yao vibaya kwa kupitisha kampuni ya M/S Hindusthan Engineering and Industries Limited kufanya ukarabati huo na kuisbabishia kupata faida.

Washtakiwa walikana mashitaka yao. Upande wa jamhuri ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na haukuwa na pingamizi la dhamana.

Hata hivyo, mshtakiwa wa kwanza, tatu, nne na wa 11 walitimiza masharti hayo na kesi hiyo itatajwa februari 25, mwaka huu.

Washtakiwawaliopandishwa kizimbani ni pamoja na Jasper Kisiraga, Mathias Massae, Muungano Kaupunda, Ngoso Ngosomwiles, Paschal Mafikiri, Kedmon Mapunda, Felix Kashaigili, Lowland Simtengu, Joseph Syaizyagi na Charles Ndenge.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.