WAZIRI WA UJENZI PROF MBARAWA AMSIMAMISHA KAZI MENEJA WA FEDHA WA ATCL.
Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Prof Makame Mbarawa
amemsimamisha kazi meneja wa fedha wa shirika la ndege Tanzania ATCL Bw.
Steven Kasubi kufuatia upotevu wa fedha zaidi ya sh. milioni mia saba
ambazo zilitokana na uuzwaji wa tiketi za ndege.
Waziri Mbarawa ametoa taarifa hiyo jijini Dar es Salaam ambapo
amesema wizi huo umefanywa kwa kushirikiana na wafanyakazi wa shirika
hilo kupitia kampuni ya wakala wa ukatishaji tiketi ya salama World
Travel iliyopo visiwa vya komoro.
Aidha amesema amemwagiza mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za
serikali (CAG) kufanya uchunguzi kwa mawakala wengine wote wa shirika
hilo kubaini kama fedha za uuzaji wa tiketi hizo zinarudishwa kama
inavyotakiwa.
Wakati huohuo waziri Mbarawa amekutana na sekta binafsi ili kujadili kwa pamoja changamoto zinazoikabili na namna ya kuzitatua.
No comments: