Ads Top

Kitwanga: Hata nikijamba Ushuzi Mtaandika.

Na mwandishi wetu Antony Sollo Misungwi.
MBUNGE wa jimbo la Misungwi Charles Kitwanga amesema kuwa kwa sasa hahitaji kuongea chochote na waandishi wa Habari maana ni wambea kwani hata akijamba ushuzi wataandika.

Mbunge huyo alitoa kauli hiyo sept 15 majira ya saa 2: 30 nyumbani kwake Usagara baada ya waandishi kufika nyumbani hapo kufuatia mwaliko wa kukutana naye kwa lengo la kutolea ufafanuzi masuala mbalimbali ikiwemo kero ya maji inayowatesa wananchi wa Usagara na vitongoji vyake kufuatia kupanda kwa bei ya maji na kufikia shilingi 500 kwa ndoo ya lita 20 na hata hivyo hayapatikani.

 “jamani waandishi nimeshachoka siwahitaji maana hata kama nikijamba ushuzi mtaandika kwa hiyo mimi sina hamu kabisaya kuonana nanyi”.alisema Kitwanga.
Baada ya waandishi hao kufika tu na kuonana na Kitwanga waliambulia maneno hayo ambapo  alisema hahitaji kuongea jambo lolote kwa kuwa waandishi wamekuwa wakiandika umbea dhidi yake.

Walipomkumbusha kuwa kulikuwa na ahadi ya kukutana kwa ajiri ya kutolea ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo Kitwanga alisema aliona atoe ahadi hiyo jana kuepusha maswali toka kwa mwandishi aliyempigia simu kupata majibu ya maswali aliyoulizwa.
“Nilikuwa na watu kwenye gari nikaona nirahisishe tusiendelee kupoteza muda ila nasema sihitaji kuongea chochote na waandishi ninyi ni wambea hamna dogo jamani aaaah sitaki rudini tu nyumbani mkaendelee na shughuli zingine”alisema Kitwanga.

Wandishi walitembelea miradi mbalimbali katika Kijiji cha Sanjo na kuambiwa kuwa kuna ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma katika miradi hiyo ambayo Kitwanga ni mmoja wa viongozi waliochangia kiasi kikubwa cha fedha kufikia mil 6 ili kukamilisha miradi hiyo ambapo hata hivyo  akionyesha msimamo wake Kitwanga hakutaka kuzungumza chochote.

Katika mradi uliotembelewa na waandishi hao walibaini kujengwa chini ya kiwango kwa vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Msingi Sanjo ambapo kabla ya kuhamia kwa wanafunzi shuleni hapo tayari vyumba hivyo vimeshachakaa huku viongozi wa Kijiji cha Sanjo wakiwaamuru wananchi kuchanga fedha kiasi cha 6500 kwa ajiri ya ukarabati jambo ambalo huenda likaibua mgogoro mkubwa kijijini hapo.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.