Ads Top

SERIKALI YATENGA BILIONI 515 KWA HALMASHAURI NCHINI KUFANIKISHA UTOAJI ELIMU BURE.

 Serikali kupitia wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia na ufundi imetenga Bilioni 515.5 kwa halmashauri zote nchini katika kufanikisha utekelezaji wa utoaji elimu bora kwa shule za msingi na Sekonndari,huku waziri wa  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mh.George Simbachawene amesema serikali haitasita kuwachukulia hatua  maafisa wa elimu na wakurugenzi katika halmashauri watakaokuwa sio waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika hafla ya utoaji wa zawadi  kwa Halmashauri zilizofanya vizuri katika sekta ya elimu hapa nchini waziri Simbachawene amesema ni wajibu kwa maafisa elimu na wakurugenzi katika Halmashauri kufanya kazi zao kwa weledi na kwa wakati kama ilivyokusudiwa.
 
Awali waziri wa Elimu,Sayansi Teknolojia na Ufundi Mh.Dk,Joyce Ndalichako alikabidhi zawadi kwa Halmashauri 10 zilizo fanya vizuri kati ya 167,ambapo Halmashauri ya Mbinga imekuwa ya kwanza na kukabidhiwa fedha kiasi cha shilingi milioni 331 wakati Halmashauri ya Makambako ikiwa ni ya mwisho katika Halmashauri zote hapa nchi na kukabidhiwa kiasi cha shilingi milioni 28.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.