Ads Top

Mwanza: Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) umeitaka polisi kufuata taratibu za kuhoji waandishi wa habar

 
Iwapo kuna jambo wanataka kujua ama hawaridhiki nalo badala ya kukamata waandishi husika na kuwahoji kwa siri huku likiwazuia kutoa taarifa za mahojiano yao.

Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan alisema kawaida habari yoyote ambayo inakuwa imetumika katika chombo cha habari, iwe na matatizo ama laa wanaopaswa kuisemea ni wahariri na siyo waandishi wa habari.

Kwa hali hiyo ameitaka Polisi kuacha kuwahoji waandishi badala yake wawasiliane na wahariri wa vyombo husika.

“Tumestushwa sana na hatua hii ya Polisi, na kutokana na kuwapo kwa taarifa za polisi kuwazuia wanaohojiwa kueleza walichohojiwa jambo hili limezidi kuzua shaka na kutufanya kuamini huenda hatua za kuwahoji waandishi wa habari Mtwara zina lengo la maalumu kwa tasnia ya habari ama ni sehemu ya mkakati wa kufinya uhuru wa habari,” alieleza.

Karsan alisema kitendo cha Polisi kumhoji mwandishi namna hiyo ni makosa, na kusema iwapo walikuwa na jambo ambalo walidhani haliko sawa kwa habari za waandishi hao walipaswa kupeleka kwa wahariri au uongozi wa Klabu za Waandishi wa Habari mikoani.

Polisi wanawahoji waandishi na watangazaji wa redio kutokana na vurugu zilizotokea Januari 26 mwaka huu na kuendelea kwa nyakati tofauti maeneo mbalimbali.

Mahakama na Halmashauri ya Wilaya ya Masasi pamoja na magari 18 na pikipiki saba ziliteketezwa kwa moto na wananchi ambao walidaiwa kupinga mradi usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es salaam.

Kwa mujibu wa taarifa toka Mtwara ilielezwa kuwa waandishi ambao mpaka sasa wamehojiwa ni Andrew Mtuli wa Redio Pride FM, ambaye anadai kuendesha kipindi cha Amka na Pride kinachorushwa na redio hiyo kila siku alfajiri.

Wengine ni Emanuel Msigwa , Hasad Mdimu, Philip Lulale na Mwandishi wa Magazeti ya Mwananchi Communications Limited, Abdallah Bakari ambaye alitarajiwa kuhojiwa.     

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.