Ads Top

Sheha wa Shehia ya Tomonda Wilaya ya Magharibi Zanzibar Mohammed Kidevu, mchezaji wa Zamani wa Timu ya KMKM , Yanga na Timu ya Taifa ya Zanzibar Kidevu Amwagiwa Tindikali na Watu Wasiojulikana

Sheha wa Shehia ya Tomonda Mohammed Kidevu akiwa katika wodi ya Hospitali kuu ya Rufaa MnazoMmoja akipata matibabu ya majaraha ya kitu kinachosadikiwa kwa Tindi Kali,akipata matibabu hayo katika hospitali hiyo.
 Sheha wa Shehia ya Tomonda Wilaya ya Magharibi Mohammed Kidevu, mchezaji wa Zamani wa Timu ya KMKM , Yanga na Timu ya Taifa ya Zanzibar Kidevu usiku wa kuamkilia leo amemwagiwa tingi kali na Watu wasiojulikana akiwa katika maeneo ya kwakehuko Tomondo jana usiku, akipatiwa matibabu katika hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja alikolazwa kwa matibabu na uchunguzi zaidi wa kitaalamu katika Hospitali hiyo. 
Sheha Mohammed Omary Said aliyemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana akiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja akipatiwa matibabu, Sheikh Mohammed amepata maumivu makali sehemu za kifuwa na jicho kuumia Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mukhadam Khamis,amesema chombo kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la tukio na kwamba polisi imekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili kugundua aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole.Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.