Ads Top

Wiki kadhaa zimepita tangu mwanamuziki mkongwe, Juma Kassim Nature atangazwe katika vyombo mbalimbali vya habari kuwa aliwahi kulewa na kuhudhuria mahojiano aliyotakiwa kufanyiwa katika kituo kimoja cha redio nchini.

 

Akizungumza na Mwananchi, Nature aliweka wazi kuwa alikunywa pombe lakini hakulewa kama inavyodaiwa licha ya kwamba alivaa ndala alivyokwenda katika mahojiano hayo.
“Ningependa mashabiki wangu wafahamu na kuelewa kwamba lile tukio ambalo limenitokea katika kituo kimoja cha redio katika mahojiano yale kwa madai kwamba nilikuwa nimevaa ndala, pia nilikuwa tayari nimeshalewa si kweli,” alisema Nature.
Hata hivyo, msanii huyo alikiri wazi kuwa alikunywa pombe lakini aliweza kujimudu hata kuendesha gari lake kutoka nyumbani kwake hadi studio.
“Endapo mtu amekunywa pombe kisha akawa bado anaufahamu wa kuweza kwenda mahali na kujielezea mpaka kuendesha  gari, huyo mtu hajalewa ila tunasema kwa lugha nyepesi amekunywa.
“Nafahamu kwamba msanii ni kioo cha jamii.  Kila msanii wa fani yoyote huwa anakuwa na staili yake ya kutoka au kwa hapa nchini tunasema ‘nitoke vipi’, sasa mimi nashangaa leo wanasema Kiroboto kavaa ndala wakati wamesahau kuna mastaa wakubwa tena wenye majina duniani wanavaa vitu ambavyo huwezi hata ukaviongelea. Mfano mzuri ni mwanadada Lady Gaga ingekuwa yule ndiyo yupo Bongo na akaenda kwenye mahojiano na vazi la nyama kama lile alilovaa, wangemtoa?
Akimalizia Nature aliweka wazi kuwa ameshatangaza kusitisha kupeleka kazi zake katika kituo hicho, pia kuwataka waache kuzirusha hewani kazi zake.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.