Wapiganaji wa kundi la Boko Haram, wamewaua watu wanne na kuteketeza nyumba zao
Wapiganaji wa kundi la Boko Haram, waliwaua watu wanne na kuteketeza nyumba zao mjini Izghe siku ya Jumamosi.
Wiki moja kabla ya shambulizi la Jumamosi , zaidi ya watu miamoja waliuawa katika eneo hilo.
Seneta Ali Ndume, alikosoa jeshi kwa kukosa kutuma vikosi katika eneo hilo baada ya shambulizi la kwanza.
Aliongeza kuwa mkakati wa serikali kuhusu usalama na ulinzi umekosa kufaulu.
Serikali ya kitaifa imekosolewa kwa kukosa
kuchukua hatua na hata kukosa kuonyesha wasiwasi wowote kuhusu
mashambulizi ya Boko Haram dhidi ya watu wasio na hatia.
Boko Haram wamesababisha vifo vya maelfu ya watu tangu mwaka 2009
Habari na BBCswahili.com
No comments: