Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Chupuchupu kutolewa nje ya Kikao cha Baraza
Na
Antony Sollo Busega.
Julai
27 2014.
Madiwani na
Wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega wamenusurika kutolewa nje
ya ukumbi wa kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa
Lunala katika mji wa Lamadi Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.
Akifungua kikao cha Baeaza la Madiwani na Wataalamu wa Halmashauri hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri
ya Wilaya ya Busega Charles Lukale alitoa onyo kali kufuatia Madiwani na
wataalamu wa Halmashauri hiyo kupuuza agizo ambalo amekuwa akilisisitiza mara
kwa mara kwao kuhusu kuvaa nguo zenye hadhi katika kikao cha Baraza hilo.
“Ndugu zangu wajumbe, naona mmeshindwa kunielewa! nimekuwa
nikiwasisitiza kila mara mvae nguo ambazo zinapaswa kuvaliwa katika kikao kama
hiki yaani nguo zenye hadhi na staha, lakini sasa naona hatuelewani napenda
niwafahamishe kwamba leo nilikuwa nimepanga kuwatoa nje ya kikao hiki ili iwe
fundisho katika vikao vingine muweze kutii maagizo leo nawasamehe! Kikao
kijacho sitakuwa na salia mtume nitamtoa nje mtu yeyote ambaye hatakuja amevaa
nguo za hadhi ( suit )” alisema Lukale.
Baada ya kutoa kauli hiyo Lukae alikifungua kikao cha
baraza hilo na kuendelea kupitisha ajenda zilizokuwa mbele ya wajumbe wa baraza
hilo.
Katika hali isiyo ya kawaida na ambayo ilileta changamoto
kubwa ni baadi ya wajumbe wa kamati ya fedha kujitokeza kuuliza maswali katika
kikao hicho wakati wao ndiyo walitakiwa kumsaidia Mwenyekiti kufafanua baadhi
ya mambo ambayo yangeibuliwa katika kikao hicho jambo lililomfanya Mwenyekiti
wa Halmashauri hiyo Charles Lukale kusimama na kutoa onyo kwa wajumbe hao na
kuwaambia ni muhimu wasome kanuni na kuelewa nini ni wajibu wa wajumbe wa
kamati.
Swali lililoulizwa na mmoja wa wajumbe wa kamati ya fedha
wa baraza hilo ni kuhusu mradi wa Umeme
unaotekelezwa katika jimbo la Busega kwamba utatekelezwa katika vijiji
vingapi.
Ambapo swali hilo lilijibiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri
ya Wilaya hiyo Yuna Hamis kwamba, Jimbo la Busega lina vijiji 55 lakini vijiji
ambavyo vitapatiwa umeme ni 46 ambapo
Mkurugenzi huyo alisema kuwa katika utekelezaji wa mradi wa umeme ni Wilaya ya
kwanza nchi nzima kufauru kutekeleza mpango wa kuwapatia wananchi umeme.
Kuhusu vitambulisho vya hudum ya Afya kwa Wazee, Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega aliesema, awamu ya kwanza vitatengenezwa
vitambulisho 1000 kwa wazee hao Wilayani
Busega.
Suala lingine lililotaka kuteka kikao cha Baraza hilo ni
kuhusu suala la mbegu feki za Pamba zinazodaiwa kutolewa kwa wakulima zikiwa
hazina ubora ambapo Mkurugenzi alisimama na kutolea ufafanuzi kuwa suala hilo akisema kuwa linakuzwa tu.
“ ndugu zangu mimi
nashangaa sana, suala hili linakuzwa mno
sisi tulimwita mhusika na kujadiliana naye na wataalamu wetu ninavyofahamu mimi, asilimia 98% ya mbegu za pamba ziliota huku asilimia 2%
tu ikishindwa kuota mimi naomba muelewe, suala hili linakuzwa tu na halina
ukweli” alisema Yuna.
Baraza la Madiwani na Wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega
lilihudhuriwa na Madiwani na wataalamu wa Idara mbalimbali lakini pia wanachi
wa kawaida walifika kuja kusikiliza ambapo Mbunge wa Jimbo la Busega ambaye
pia ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dk Titus Kamani alihudhuria Kikao
hicho.
No comments: