Ads Top

Mvua yaleta kizaazaa jijini Mwanza

Baadhi ya magari yaliyozingirwa na maji katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza baada ya Mvua kubwa kunyesha julai 26 mwaka huu. Picha na Antony Sollo



Na Antony Sollo   Mwanza
Julai 26 2014.
Mvua iliyonyesha julai 26 jijini Mwanza imeleta kizaazaa na kusababisha Mkutano wa Naibu katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi mwigulu Nchemba kuingia dosari,mvua hiyo iliyoanza kunyesha majira ya saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana,imesababisha taharuki kubwa kwa wakazi wa jiji la Mwanza na Vitongoji vyake hii ni baada ya maji kujaa na kusababisha baadhi ya barabara kukatika na kusababisha usafiri kuwa wa shida jijini humo.

Wakizungumza na Tanzania Daima, wananchi waliokuwa jirani na uwanja huo, walisema mvua hiyo haijawahi kunyesha kwa kipindi chote cha masika kwa msimu wa 2014.

Mvua hiyo pia imesababisha baadhi ya mabomba ya maji katika uwanja wa CCM Kirumba kupasuka na kusababisha huduma mbalimbali kukwama.

Akizungumzia mazingira ya uwanja wa CCM Dereva mmoja wa gari la Chama cha Mapinduzi aliyesema kuwa hatapenda kuandikwa gazetini alishangazwa na kuanza kutoka maji katika uwanja huo jambo ambalo si la kawaida kufuatia kukatwa kwa maji katika Uwanja huo baada ya wamilki wa uwanja huo kushindwa kulipa bili za maji.

“Au kwa kuwa Naibu Waziri yuko hapa ndiyo kasababisha maji haya yatoke? alihoji Abdalla Nasoro ambaye ni mmojs wa wanachama wa CCM”

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.