Serikali kutoa Ruzuku kwa Vikundi vya Wavuvi
Na Antony Sollo Busega.
Julai 26 2014.
Serikali itaanza kutoa Ruzuku kwa wavuvi watakaokuwa katika
vikundi vilivyosajiliwa, ambapo fedha hizo zitatolewa kwa ajili ya kununua zana
za uvuvi ikiwamo mitumbwi ya kisasa pamoja na nyavu ili kuondoa tatizo la uvuvi
haramu na kuwafanya wananchi wafanye kazi zao kihalali na kwa uhuru.
Kauli hiyo ilitolewa na Mbunge wa Jimbo la Busega ambaye
pia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dk Titus Kamani kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika
julai 21 mwaka huu katika kijiji cha
Ijitu kata ya Kiloleli.
Akiwahutubia wananchi waliokuwa na hamu ya kujua ujio wa
Mbunge wao Dk Kamani aliwaomba wananchi kuchangamkia fursa hii ili waweze
kujiajili ,lakini pia waweze kujipatia mahitaji yao na kupambana na umaskini,
Alisema kuwa Serikali itatoa ruzuku ya asilimia arobaini
huku wanakikundi wa ushirika wa wavuvi hao wakichangia asilimia sitini “ jamani
ndugu zangu wananchi hii ni fursa iliyotolewa na Serikali ili muweze kupata
ruzuku kwa ajili ya kununua zana za kisasa ili muondokane na zana ambazo
zinaingizwa isivyo halali maana mtakuwa mnafanya kazi zenu mkiwa huru.
Akijibu swali aliloulizwa juu ya kulipa mapato mara mbili
au zaidi wakati tayari alishakata leseni Dk Kamani aliwaambia tatizo hilo amelirithi
toka kwa watangulizi wake akiwemo Waziri John Pombe Magufuli na kuahidi
kulitafutia ufumbuzi suala hilo ili kuondoa urasimu huo
“ ndugu zangu naomba
muelewe,kila halmashauri nchini ina vyanzo vyake vya mapato,sasa huwezi kukata
leseni Bunda ukaenda kufanya kazi mpaka Ukerewe kwa leseni ileilie, na suala
hili limetuumiza sana kichwa hivyo Serikali inajitahidi kulitafutia ufumbuzi
mapema iwezekanavyo”alisema Dk Kamani.
Waziri Dk Kamani alitoa msaada wa baiskeli mbili za
magurudumu manne kwa ajili ya walemavu, ili ziweze kuwasaidia kwenda sehemu
mbalimbali na baada ya hapo aliwashukuru wananchi kwa kumchagua na kuwaomba
ushirikiano ili waweze kuleta maendeleo jimboni humo.alikemea vitendo vya
majungu na kusema kuwa kipindi hiki ni cha kazi maneno hayataweza kuleta
maendeleo
Natambua kuwa walemavu nao ni binadamu kama ilivyo kwa
binadamu wengine,ninatoa baiskeli hizi ambazo nimezipata kutoka kwa marafiki
zangu wa shirika la Desk and Chair kwa ajili ya walemavu waliomo katika jimbo
letu hivyo naomba mzitumie vizuri”.alisema Dk Kamani.
Mwisho.
No comments: