Ads Top

TAMKO RASMI LA CHADEMA KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA MPYA

 
 Mhe.Tundu Antipus Lissu,Mjumbe Kamati Kuu,CHADEMA.
Mhe.Freeman Mbowe!
"Mchakato wa Katiba ni mchakato wa Kisiasa.
Mchakato ukiharibiwa, hutengeneza Ombwe.
Makundi mbalimbali yamekuwa yakitoa wito ili kuokoa mchakato wa Katiba.
Rai ya kututaka UKAWA kurudi bungeni, bado haijazingatia yale yaliyotufanya tutoke Bungeni.
Viongozi wa UKAWA tumekaa na kujadili kwa kina.

Ni uwendawazimu kurudi bungeni kwa mazingira yale yale.
UKAWA tumechukua nafasi kuziba Ombwe la uongozi wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi.
Tuna ushahidi wa namna CCM wanavyopanga kuvuruga mchakato wa Katiba.
Sisi tutapanga namna ya kuandaa Plan B.
Hatuko tayari kwenda kwenye uchaguzi Mkuu mwakani kwa Sheria hizi hizi.

Siku ya Jumapili baada ya vikao hivi, tutatoka na maazimio na tutaongea na vyombo vya Habari.
Tutakaa na kujadili kwa kina kwenye vikao hivi vya leo na kesho, pamoja na agenda nyingine, lakini ni lazima tutoke na maamuzi mazito.

Tunamtaka Rais aache tabia ya ukigeugeu.

Tunamtaka Rais kwa muda mchache aliobakia madarakani, ajifunze hata kwa kujilazimisha, aache tabia ya unafiki".

Mhe.Mbowe ameyasema hayo kwa niaba ya Chama katika hotuba yake fupi ya ufunguzi wa vikao vya Kamati Kuu ya CHADEMA vinavyoendelea hivi sasa katika Ukumbi wa Mbezi Garden Hotel iliyopo Mbezi Beach Jijini Dar Es Salaam.

Mhe.Tundu Antipus Lissu,
Mjumbe Kamati Kuu,
CHADEMA.
18/07/2014.
Ahsanteni sana!!!

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.