Ads Top

MAWAZIRI AMBAO HAWAJAJAZA FOMU ZA MAADILI WAPEWA SAA 12 KUJAZA FOMU HIZO.

Saa chache tangu waziri mkuu Mh Kassim Majaliwa atangaze majina ya mawaziri wanne na naibu waziri mmoja kuwa wanatakiwa kuwasilisha fomu zao za  maadili ya utumishi ya ummaa na mali wanazomiliki katika ofisi ya tume ya taifa ya maadili la sivyo watakuwa mawejionda wenyewe katika nafasi zao waziri wa mambo ya ndani Mh Charles Kitwanga ambaye ni mmoja ya mawaziri waliotajwa amesema amesikitihwa sana na kitendo cha kutajwa jina lake kuwa hajarudisha fomu zake wakati amekwisha fanya hivyo muda mrefu.

Akizungumza na waandishia wa habari Mh Majaliwa amesem ameagizwa na rais John Magufuli kuwa wale wote mabo wamekiuka sheria na kuacha kujaza na kurudisha fomu hizo awataje na kisha watekeleze agizo hilo ndani ya saa kumi na mbili.
 
Hata hivyo baada ya kutolewa kwa tangazo hilo ITV ilipiga kambi katika ofisi za tume ya maadili kwa lengo la kuweza kubaini kama kuna waziri ambaye ataitikia agizo hilo na ndipo ilipofika saa 6:45 alikuja Mh Kitwanga ambaye alisema ameshangaa kuona jina lake limetajwa na hivyo anakwenda katika ofisi za tume hiyo kutoa malalamiko yake.
 
Ilipofika saa 7:05 mchana naye waziri wa mambo ya nje, ushirikiano wa Afrika Mashariki, kikanda na kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ambaye alikiri kutorudisha fomu hizo kutokna na kuwa na majukumu mengi.
 
Kabla ya kwenda katika ofisi za tume kituo hiki kilikwenda katika ofisi za naibu waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira na muungano Mh Luhaga Mpina saa 5:30 ambaye hakunonekana kuwa na taarifa za agizo la waziri mkuu na baada ya kupewa taarifa na mwandishi akakiri kurudisha fomu hizo kwa sababu alipoteuliwa hakuwa anajuwa mshahara wake na stahiki zingine lakini sasa anajuwa ataipeleka.
 
chanzo ITV

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.