Ads Top

SERIKALI YAWATAKA WATENDAJI TRA KUACHA KUWATISHA WAFANYABIASHARA MKOANI KILIMANJARO.

Waziri wa fedha na mipango Mh Dr. Philp Mpango amesema hakuna mtendaji wa serikali aliyejinufaisha na mapato ya serikali atakaye samehewa na hakuna mtendaji mwadilifu atakayeonewa.

Mh .Dr Mpango ameyasema hayo alipokuwa anazungumza na watendaji wa kituo cha pamoja cha forodha cha Holili mkoani Kilimanjaro.
 
Aidha amewataka maafisa wa TRA kukufanyakazi kwa uadilifu na kuacha kutumia kampeni zinazoendelea za kudhibiti mapato kuwatisha wafanyabiashara badala yake wawasaidie waweze kuzalisha na kulipa kodi halali.
 
Aidha amewataka watendaji wa mamlaka ya mapato ambao bado hawajatangaza mali zao wanazomiliki kufanya hivyo mara moja kwani hakuna njia ya mkato lazima lengo la serikali la kuisafisha mamlaka hiyo mbele ya jamii litimie.
 
Kuhusu malalamiko ya kuendelea kuwepo kwa usumbufu wa baadhi ya watendaji wanaotumia nyadhifa zao kuwasumbua na wasafirishaji wa bidhaa na kuwawekea vikwazo barabarani Dr Mpango amesema siku zao zinahesabika na amewataka wananchi na watumishi wadilifu kuwafichua kwani wanawasababishia watu wengine matatizo.
 
Meneja wa TRA mkoa wa Kilimanjaro Bw Abdul Mapembe amesema ukusanyaji wa mapato unaendeleabkuongezeka siku hadi siku licha ya kuwepo kwa baadhi ya changamoto ikiwemo ya uhaba wa vitendea kazi.
 
Kwa sasa ukusanyaji wa mapato umeongezeka kutoka bilion mia tisa hadi kufikia trilion 1.6 kwa mwezi.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.