Ads Top

ZAIDI YA HEKARI 400 ZA MAZAO ZIMEHARIBIWA NA MVUA YA MAWE BUKOMBE.

Zaidi ya hekari 400 za Mahindi, Mihogo na Pamba zimeharibiwa vibaya na mvua ya mawe katika kijiji cha Ng’anzo wilaya ya Bukombe mkoani Geita na kusababisha hasara kubwa kwa wakulima waliokopeshwa pembejeo na mbegu katika msimu huu wa kilimo.

ITV imeshuhudia shamba la Mahindi katika kitongoji cha Nyakato kijijini humo likiwa limeharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani Bukombe, huku diwani wa kata ya Ng’anzo Kipara Siyantemi akiililia serikali kuwatazama kwa jicho la huruma wakulima hao ambao mazao yao yameathirika.
 
Kando na athari hizo za mvua, wakazi wa kijiji hicho cha Ng’anzo wanalia na ubadhirifu wa fedha za ujenzi wa zahanati, upotevu wa mifuko 100 ya saruji, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini katika mgodi wa Nsagali pamoja na barabara. 
 
Kilio hicho kinapatiwa majibu na mbunge wa jimbo la Bukombe Mh. Dotto Mashaka Biteko.
chanzo na ITV
 

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.