Ads Top

WAKAZI ZAIDI YA 150 GONGOLAMBOTO WATALAZIMIKA KULALA NJE BAADA YA NYUMBA ZAO KUBOMOLEWA.

Wakazi zaidi 150 wa Guluka kwalala Gongolamboto jijini Dar es Salaam ambao nyumba zao 25 zimebolewa wamesema kwa sasa watalazimika kulala nje kwa kukosa nyumba za kuishi baada ya zoezo la bomoabomoa kufanywa na uongozi wa kiwanda cha kampuni ya NAMERA huku wakazi hao wakisema zoezi zima la ubomoaji limefanyika wakati kesi kuendelea kusikilizwa katika mahakama ya ardhi.

Wakiongea na ITV mara baada ya kufika katika eneo hilo la Guluka kwalala na kushuhudia mabaki ya nyumba ambazo zimebomolewa wananchi hao wamelalamikia zoezi zima la ubomoaji wa nyumba hizo baada ya idadi kubwa ya wakazo hao kushindwa kutoa samani zao ndani wakati zoezi la ubomoaji likifanyika na kusimamiwa na askari wa jeshi la polisi.
 
Bwana Fitiri Juma ambaye ni mjumbe wa seikali ya mtaa wa Guluka Kwalala akiongea na ITV amelalamikia viongozi wote wa eneo hilo kutofika wakati zoezi la ubomoaji likendelea na kusababisha wananchi hao kupata hasara ya mali zao.
 
Katika kutaka kujua juu ya uhalali wa zoezi zima la ubomoaji kama limezingatia misingi ya sheria ITV iliutafuta uongozi wa kiwanda cha NAMERA ambapo uongozi umekiri kutelezela zoezi hilo na kulipa fidia wananchi wote waliojenga eneo hilo wanalodai ni la kiwanda.
Chanzo ITV

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.