WIZARA YA FEDHA IMEIPATIA IDARA YA MAHAKAMA SH BILIONI 12.3 KUBORESHA UTENDAJI KAZI.
Wizara ya fedha imetimiza ahadi ya rais Dr. John Magufuli aliyotoa
siku nne zilizopita kwa idara ya mahakama wa kuipatia idara hiyo
shilingi bilioni 12.3 ili ziweze kusaidia uendeshaji wa mahakama nchini
hasa usikilizaji wa kesi zinazohusiana na kodi.
Fedha hizo zimekabidhiwa kwa idara ya mahakama na waziri wa fedha
na mipango Dr.Philip Mpango ambapo amesema serikali inatumaini utendaji
kazi wa mahakama sasa utafanyika kwa kasi zaidi.
No comments: