AFISA BIASHARA MANISPAA YA UBUNGO AWALIZA MAMILIONI WAFANYABIASHARA
Na Antony Sollo Ubungo.
AFISA
biashara wa Manispaa hiyo Geofry Mbwama anatuhumiwa kujipatia mamilioni ya
fedha toka kwa wafanyabiashara wenye maduka pamoja na wajasiriamali katika manispaa
hiyo baada ya kuingia kila duka akiomba Leseni ya biashara akiwa na Dereva wa
Manispaa hiyo na kufanikiwa kujipatia kiasi kikubwa cha fedha akitumia nyaraka
bandia za Serikali Tanzania Daima libaini.
Tukio hilo
lilitokea desemba 13 mwaka jana katika Mtaa wa Mbezi Luis Manispaa ya Ubungo
Jijini Dar Es Salaam ambapo Mbwama akiwa na gari la Manispa hiyo aliingia
katika maduka na vibanda vya wafanyabiashara wadogo mafundi pikipiki hata
wanaofanyia shughuli zao nje huku akihoji kama wana Leseni za biashara na pale
ambapo alikuta hawana kwa sababu mbalimbali alifunga biashara na makufuli yake
na baadaye aliandika nyaraka inayodaiwa kuwa ni feki na kuwapiga faini kati ya
321,000.
Akithibitisha
kufanyiwa vitendo hivyo mmoja wa wajasiriamali (Fundi pikipiki) eneo la Mbezi
makabe road Rahesh Shaban ambaye anajishughulisha na ufundi wa pikipiki alisema
alilazimishwa kufunga shughuli zake baada ya kubainika kuwa hakuwa na leseni ya
kufanya kazi ya ufundi licha ya kujitetea kuwa alikuwa ameenda katika
mamlaka ya Mapato Tanzania kwa ajili ya kupatiwa namba ya utambulisho wa mlipa
Kodi ( TIN Number) lakini Afisabiashara huyo alimwandikia faini ya shilingi
321,000 na kumwamuru afunge shughuli zake.
“Mimi na
wenzangu hapa tumemweleza kuwa tunazo baadhi ya nyaraka na kwamba tayari
tulikuwa tumeshaanza mchakato wa kupatiwa namba ya utambulisho ya mlipa kodi(
TIN Number) lakini hakutuelewa na matokeo yake aliandika faini katika nyaraka
ambazo tunahisi ni feki kwa kuwa nyaraka yoyote ya Serikali huwa haiandikwi kitu
chochote au namba ya mtu binafsi ambapo hata hivyo aliomba fedha kiasi kati ya
20,000, mpaka 60,000 tukampatia na hakutoa risiti yoyote”alisema Shabani.
Kwa kuwa
Shaban aliona kuwa mahala pale ndipo anapopata riziki kwa ajili ya mahitaji ya
familia yake,aliomba asamehewe lakini kilichoshangaza aliombwa shilingi 20,000
na Mbwama lakini hakupatiwa risiti jambo ambalo pia lilithibitishwa na
wafanyabiashara wa duka la madawa yaliyoko jirani na Shabani ambao nao walitoa
fedha kiasi cha shilingi 60,000 kila mmoja kutokana na kutishiwa kufungiwa
maduka yao ambapo fedha hizo zilikabidhiwa kwa dereva wa Manispaa ambaye naye
alikuwa akiwakaripia wafanyabiashara na kutoa vitisho vya kuwafungia biashara
zao.
Tanzania
Daima lilifuatilia nyendo za Mbwama na kukutana na malalamiko lukuki kwamba
wafanyabiashara na wajasiriamali wa Mtaa wa Mbezi walio wengi walikuwa
wameshachukuliwa fedha zao kutokana na tishio la kufungiwa biashara zao na
Afisa biashara huyo akishirikiana na dereva wake.
Mwandishi wa
gazeti la Tanzania Daima alimtafuta Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo ambapo
hata hivyo juhudi za kumpata Mkurugenzi huyo ziligonga mwamba kutokana na
mwingiliano wa majukumu ambapo lilikutana na Katibu Tawala James Mkumbo ambaye
baada ya kupatiwa taarifa juu ya kilichofanywa na watumishi hao dhidi ya
wafanyabiashara nawajasiriamali na kuahidi kuzifanyia kazi tuhuma hizo ambapo
tangu 13 desemba hadi leo hakuna taarifa zozote.
Mara kadhaa
Mkumbo amekuwa akitakiwa kutolea ufafanuzi wa tatizo hilo lakini amekuwa akidai
kuwa alikabidhi watu kufanyia kazi tuhuma hizo
“Kwa sasa
niko Mwanza lakini kuna watu niliwapa jukumu la kushughulikia suala hilo lakini
pia sisi hatufanyi kazi kwa pressure za waandishi wa Habari kwa sababu wanataka
habari tukikamilisha utaratibu wetu tutafanya kinachostahili ”alijibu
Mkumbo kwa njia ya ujumbe wa simu ya mkononi.
Kinachoshangaza
hapa ni kwamba hakuna taarifa zozote kuhusu ufuatiliaji wa tuhuma hizi pamoja
na Katibu Tawala huyo kupelekewa Ofisini tuhuma zinazowakabili Afisa biashara
wa Manispaa pamoja na dereva wa Manispaa ya Ubungo kwa takribani miezi miwili
sasa jambo linalozua sintofahamu juu ya uadilifu wa watumishi hao
Wananchi
waliozungumza na gazeti hili wameiomba Serikali kuwachunguza baadhi ya
wafanyakazi wake hasa waliotumbuliwa kwa kuwa sasa wengi wako mtaani hawana
kazi na wamegeuka Matapeli wanaotumia mbinu walizokuwa wamezizoea wakiwa kazini
kutafuta fedha kwa njia za vitisho na inasemekana Mbwama na dereva wa Manispaa
ya Ubungo kwa pamoja wamejipatia mamilioni kwa njia hiyo.
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Ubungo John Kayombo hakuwez kupatikana mara moja kuzungumzia
tuhuma hizo ambapo juhudi za kumtafuta atolee ufafanuzi wa hatua gani
zimechukuliwa dhidi ya tuhuma kwa watumishi hao kwa kukiuka maadili ya Utumishi
wa Umma
MWISHO.
No comments: