HALI YA USALAMA JIJINI DAR ES SALAAM YAWA TETE MABOMU YA MACHOZI YALINDIMA MAENEO YA KARIA KOO
Muumini wa dini ya Kiislamu akishahadia kwa mola wake na kusema nipo
tayari kufa kwa ajili ya kutetea dini ya Allah baada kukamatwa na Askari
wa Kikosi cha Kutulia Ghasia katika viunga vya eneo la Ikulu.
Askari wa Kikosi cha kutuliza Ghasia (FFU) wakimwingiza katika gari
muumini wa Kiislamu aliyekamatwa katika viunga vya maeneo ya Ikuu
Safari ya kuelekea Kituo Kikuu ilianza
Barabara ya kuingia katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
zikiwa zimefungwa na Askari Polisi kufuatia vurugu zilizotokea leo
Askari wa jiji wakishiriki kikamilifu katika zoezi la kuwakamata watu
waliokuwa wamekusanyika kwa nia ya kutaka kuandamana katika eneo la
Kariakoo
Polisi wakifanya doria kwa kutumia pikipiki
Mitaa ya Kariakoo na viunga vyake ikiwa imeimarishwa na Askari wa Jeshi
la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika mitaa ya Kariakoo leo
Wanajeshi wakivinjari katika mitaa ya Kariakoo leo
Ulinzi uliimarishwa na Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika mitaa ya Kariakoo leo
Magari ya
Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa katika doria katika barabara
yaMsimbazi ambako kulitokea vurugu zilizosababishwa na waislamu
waliotaka
kuandamana.
No comments: