Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta amewaadaa baadhi ya viongozi wanaojiita UKAWA kwa taarifa yao ya kutaka kumfikisha Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) kwa kuendeleza mchakato huo wa Katiba
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta
akiongoza bunge hilo
MWENYEKITI
wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta amewaadaa baadhi ya viongozi
wanaojiita UKAWA kwa taarifa yao ya kutaka kumfikisha Mahakama ya Kimataifa ya
Uhalifu wa Kivita (ICC) kwa kuendeleza mchakato huo wa Katiba.
Kauli
hiyo imetolewa leo 12 Septemba, 2014 mjini Dodoma na Mhe. Sitta kufuatia baadhi
ya viongozi hao, kudai kuwa watampeleka katika mahakama hiyo.
Mhe.
Sitta ameeleza kuwa baadhi ya viongozi wa kundi hilo kuwa wanakipaji kikubwa
cha uigizaji huku akifafanua kuwa wakati walipokuwa Bungeni wakati wa mchakato
wa kupiga kura za siri, viongozi wa kundi hilo walizifanya kura hizo kuwa wazi
na baadaye kuja na kauli kuwa Bunge Maalum la Katiba linaloendelea sasa sio
halali lihairishwe.
“Juzi
Mhe. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekutana nao mara mbili kwa muda wa saa
Saba na katika kukutana huko wakafikia maafikiano, lakini siku moja baadaye wao
wamekana yote waliyokubaliana hapa mjini Dodoma, kwa hiyo ni vyema wananchi
wakawapima hawa watu”, alisema Mhe. Sitta.
Aidha,
Mhe. Sitta aliasa kwa kusema kuwa wananchi na viongozi wanatakiwa kujua kuwa
mchakato wa bunge Maalum la Katiba sio jambo la mzaha na wao hawapo hapo
bungeni kwa mzaha mzaha.
“Mimi
nawaambia kuwa hapo mwakani watakaposhindwa uchaguzi basi warejee katika fani
zao ambazo Mwenyezi Mungu kawajalia”, alisema Mhe. Sitta.
No comments: