LIGI KUU ENGLAND MECHI ZITAKAZO CHEZWA KESHO 21 SEP 2013
BAADA kuburudishwa na Mashindano makubwa ya Vilabu Barani Ulaya, Wadau wa Soka laEngland
Wikiendi hii watarudi vitini mwao kuangalia Ligi Kuu England, Barclays
Premier League, BPL, ambao Timu zitakuwa zikicheza Mechi zao za 5 tokea
Msimu kuanza na mvuto mkubwa ni mtanange wa Jiji la Manchester wakati
Mabingwa Manchester United watakapotua Etihad kucheza na Mahamu wao,
Manchester City.
..........................................
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumamosi 21 Septemba
14:45 Norwich City v Aston Villa
17:00 Liverpool v Southampton
17:00 Newcastle United v Hull City
17:00 West Bromwich Albion v Sunderland
17:00 West Ham United v Everton
19:30 Chelsea v Fulham
Jumapili 22 Septemba
15:30 Arsenal v Stoke City
15:30 Crystal Palace v Swansea City
18:00 Cardiff City v Tottenham Hotspur
18:00 Manchester City v Manchester United
..............................................................
Hadi sasa Liverpool ndio wako kileleni
wakiwa na Pointi 10 baada kushinda Mechi 3, ikiwemo kuwafunga Mabingwa
Watetezi Manchester United Bao 1-0, na kutoka Sare moja.
Nyuma ya Liverpool zipo Arsenal na
Tottenham zinazofungana kwa Pointi, zote zikiwa na 9, na kisha zinafuata
Timu 5 zenye Pointi 7 kila moja na hizo ni Man City, Man United,
Chelsea, Stoke City na Newcastle.
No comments: