Vijana wa Arsene Wenger watafungua pazia la Ligi ya Mabingwa leo kwa kuivaa Marseille nyumbani kwao
Kipa wa Marseille, Steve Mandanda amewatahadharisha Arsenal kuwa katika
kundi la kifo walilopangwa wategemee kila mechi ni sawa na fainali
Gunners wanajua pamoja na kuwa na kiungo mpishi,
Mesut Ozil na mshambuliaji Olivier Giroud, bado wanakabiliwa na
ushindani mkali kutoka kwa Napoli na Borussia Dortmund katika kundi
hilo.
Kipa huyo wa kimataifa wa Ufaransa, Mandanda
alisema: “Mechi za makundi za Ligi ya Mabingwa ni ngumu. Kila klabu
inataka kusonga mbele, hivyo mechi zote zinakuwa kama fainali na ni
lazima ushinde nyumbani. Vinginevyo nafasi yako ya kusonga mbele
itapotea.
“Giroud yupo katika kiwango kizuri. Tunatakiwa
kuwazuia wasitufunge na kutokuwapa mwanya wa kucheza wanavyotaka, lakini
hiyo haitokuwa kazi rahisi kwa sababu kwa sasa wana kikosi bora.
“Uwepo wa Ozil umeifanya safu ya ushambuliaji ya
Arsenal kuwa hatari zaidi. Uwepo wake Arsenal na aina yake ya uchezaji
ni ule anaoutaka Wenger. Sikutegemea Real Madrid watakubali kumwachia
kirahi hivi aondoke.”
Madrid, Kocha wa Barcelona, Gerardo Martino
atakiongoza kwa mara ya kwanza kikosi chake kucheza Ligi ya Mabingwa kwa
kuwakaribisha Ajax Amsterdam kwenye Uwanja wa Nou Camp leo huku
akisumbuliwa na ubutu wa safu yake ya ulinzi pamoja na ufungaji. Martino
aliyerithi mikoba ya Tito Vilanova aliyewapa taji la nne la La Liga
ndani ya misimu mitano iliyopita, lakini wakiwa na kumbukumbu ya
kunyukwa mabao 7-0 na Bayern Munich katika mechi mbili za nusu fainali
ya michuano hiyo.
Macho ya mashabiki wa Barca leo yatakuwa kwa Neymar na Lionel Messi ambao wameanza kuonyesha uelewano mzuri katika uchezaji wao.
Kocha wa Ajax, Frank de Boer, si mgeni machoni mwa
mashabiki wa Barca kwani alishawahi kuichezea timu hiyo kati ya mwaka
1999 na 2003 na kutwaa taji la Ligi ya Hispania 1999 akiwa na pacha wake
Ronald.
De Boer alisema kama Ajax watafanikiwa kupata pointi yoyote Barcelona itakuwa ni mafanikio makubwa kwao.
Mechi nyingine ya Kundi H inayochezwa leo ni AC Milan dhidi ya Celtic


No comments: