Ads Top

TFDA Yateketeza samaki waliooza jijini Da es salaam

TFDA imeteketeza samaki waliooza  aina ya vibua wenye thamani ya takriban tsh 11,475,000 mali ya kampuni ya Sais Boutique.  Samaki hao walioingizwa nchini kutokea nchi ya China walikamatwa na TFDA katika eneo la Tabata Bima wakati wa ukaguzi wa bidhaa za chakula.  Kufuatia ukaguzi huo uliofanyika septemba 18, 2013 Samaki hao walibainika wakiwa wameoza na hawafai kwa matumizi ya binadamu.  Samaki aina ya vibua wamekuwa ni maarufu kuuzwa maeneo ya feri na maeneo mengine ya mjini.
Mmiliki wa kampuni ya Sais ailifunguLliwa kesi yenye namba BUG/RB/1184/2013  kwa kosa la kuhifadhi samaki ambao wameoza, kuhifadhi katika eneo ambalo halijasajiliwa na kushindwa  kutoa taarifa kwa wakaguzi wa tfda kuhusu uwepo wa samaki mpakani ambapo mtuhumiwa amehukumiwa kulipa faini ya sh. 1000, 000 na kuharibu mzigo kwa gharama zake.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.