Ads Top

PONGEZI KWA MAAFISA NA ASKARI WA JESHI LA MAGEREZA WALIOSHIRIKI GWARIDE RASMI LA MAADHIMISHO YA MIAKA 52 YA UHURU

  Gadi ya Wanaume ya Jeshi la Magereza ikipita mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama(hayupo pichani)katika mwendo wa haraka kama inavyoonekana katika picha.
  Gadi ya Wanawake ya Jeshi la Magereza ikiwa katika mwendo wa pole kama wanavyoonekana katika picha wakipita mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama(hayupo pichani).
  Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Gideon Nkana akitoa hotuba fupi kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza kwa Washiriki wa Gwaride rasmi la Maadhimisho ya Miaka 52 ya Uhuru wa Tanganyika(hawapo pichani). Hafla hiyo fupi imefanyika jana Desemba 09, 2013 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa wa Magereza, Ukonga Dar es Salaam.
 Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza walioshiriki kikamilifu Gwaride rasmi la Maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanganyika wakisakata rumba mara baada ya kumaliza shughuli ya Paredi. Hafla hiyo fupi iliandaliwa na Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja kwa lengo la kuwapongeza Makamanda hao  kutokana na umahiri,  ukakamavu waliouonyesha katika Gwaride la Maadhimisho ambapo hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi w Bwalo Kuu la Maafisa wa Magereza, Ukonga Dar es Salaam.
Baadhi ya Wataalam wa Magwaride wa Jeshi la Magereza wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza Washiriki wote wa Gwaride la Maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanganyika. Hafla hiyo fupi iliyoandaliwa na Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja kwa lengo la kuwapongeza Makamanda hao imefanyika jana Desemba 09, 2013 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa wa Magereza, Ukonga Dar es Salaam.Picha zote na Jeshi la Magereza

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.