JESHI LA POLISI LAUA MAJAMBAZI WATATU KATIKA MAJIBIZANO YA RISASI MKOANI ARUSHA.

Jeshi
 la Polisi mkoa wa Arusha limewaua kwa risasi watu watatu wanaodaiwa 
kuwa ni majambazi na kukutwa na bunduki moja aina ya AK 47 ikiwa na 
risasi kumi na nane milipuko ishirini na saba sale za jeshi la wananchi 
wa Tanzania na bendera inayodaiwa kutumiwa na kikundi cha Al Shababy 
katika tukio lililotokea eneo la Engosheraton Sinoni jijini Arusha. 
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Arusha Libaratus Sabas amesema 
jeshi la polisi lilipata taarifa ya uwepo wa majambazi hao kutoka kwa 
wasamariawema wakitaka kufanya tukio na baada ya kufika katika eneo la 
tukio watu hao walianza kurusha risasi kwa askari lakini askari 
waliwashinda nguvu na kufanikiwa kuuwa majambazi watatu ambapo mmoja 
akifaamika kwa jina la Athumani Ramadhani.
Aidha kamanda Sabas amevitaja vifaa pamoja silaa zingine walizi 
kutwa nazo majambazi hao ikiwa ni pamoja na pikipiki simu na vingine 
mapanga na visu kama anavyoeleza na baadhi ya wananchi wakilitaka jeshi 
la polisi kuendelea kuzibiti ongezeko la silaa na kuchunguza mahali 
panapo toka silaa hizo za kijeshi ambazo zimeenea katika maeneo mengi ya
 raia.
 
 
 
 
 
 
No comments: