UNCDF YAWAKUTANISHA WATAALAMU WA FEDHA KUTOKA NCHI MBALIMBALI KUJADILI JINSI YA KULETA MAENDELEO KWA KUTUMIA VYANZO VYA NDANI
Mkurugenzi
 wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa Mataifa (UNDCF), David Jackson, 
(kulia), akitoa mada kwenye mkutano wa siku mbili wa wataalamu wa fedha 
na wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali Duniani, kwenye hoteli 
ya Hyaatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Februari 29, 2016. 

Naibu
 Mkurugenzi Mtendaji Benki ya TIB, Jaffer Machano, akitoa mada kwenye 
mkutano wa siku mbili wa Wataalamu wa fedha na wadau wa maendeleo 62 
kutoka nchi mbalimbali Duniani, kwenye hoteli ya Hyaatt Regency, 
Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Februari 29, 2016.

 Mtoa Mada, Suzane Ngane kutoka Cameroun,  akitoa mada kwenye mkutano huo.
 Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT), Habraham Shemumoyo, kitoa
 mada kwenye mkutano wa siku mbili wa Wataalamu wa fedha na wadau wa 
maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali Duniani uliofanyika jijini Dar es 
Salaam, Februari 29, 2016.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT), Habraham Shemumoyo, kitoa
 mada kwenye mkutano wa siku mbili wa Wataalamu wa fedha na wadau wa 
maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali Duniani uliofanyika jijini Dar es 
Salaam, Februari 29, 2016.
Na Beda msimbe
Wataalamu  wa
 fedha na wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali duniani wameanza 
mkutano wa siku mbili jijini Dare s Salaam kuangalia namna ya  kuwezesha
 fedha za kusaidia maendeleo endelevu  kwa kutumia vyanzo vya ndani.
Mkutano
 huo wa siku mbili ulioanza jana katika hoteli ya Hyatt Regency, 
Kilimanjaro umelenga kuja na maelezo muafaka ya namna ya kupata fedha za
 kuendesha na kujenga miundombinu mbalimbali kwa ajili ya miji 
inayotanuka.
Katika
 mahojiano na mwandishi wa Mo Blog kuhusu mkutano huo , mmoja wa 
wakurugenzi wa UNCDF kutoka makao makuu anayeshughulikia uendelezi wa 
fedha, David Jackson alisema kwamba wataalamu walioalikwa wanatarajiwa 
kutoka na msimamo unahusu uwezeshaji wa fedha wa ndani.
Alisema
 wakati dunia inakabiliwa na mabadiliko makubwa ya wananchi kutoka 
vijijini kwenda mijini uwezo wa majiji mengi duniani ikiwamo manispaa ni
 mdogo kuwezesha kutengeneza miundombinu na pia kuwezesha ajira.
Alisema  kwa
 sasa kutokana na uwingi wa watu wanaofurika katika miji, 
halmashauri  na uhaba wa fedha kutoka katika vyanzo vya mapato 
kumesababisha kushindwa kuendelezwa mifumo endelevu ya miundombinu na 
ajira na kulazimisha wataalamu kuanza kuangalia namna nyingine ya kupata
 fedha.
Alisema
 mpango wa kutafuta vyanzo vingine vya fedha kwa kuunganisha nguvu nje 
ya mfumo rasmi umewezekana Tanzania hasa kutokana na manispaa kama ya 
Kibaha kuwezeshwa kupata fedha za miradi mbalimbali na wengine nao 
watatoa uzoefu wao.
“Zamani
 ilikuwa rahisi sana kwa manispaa nyingi kutengeneza mipango ya 
maendeleo, lakini kwa sasa kutokana na uwingi wahamaji vyanzo vya 
kawaida vimezidiwa na kuonekana haja ya kutafuta vyanzo vingine ili 
kuwezesha maendeleo na ajira,” alisema Jackson.
Alisema
 mataifa yanahitaji sasa kuangalia mifumo yao ya kuwezesha maendeleo 
endelevu kwa kutumia vyanzo vya ndani ambavyo vinawezekana kupatikana.
Aliongeza
 kuwa miradi mikubwa ya maendeleo haiwezi kufanywa na vyanzo vya zamani 
na kutolea mfano mradi wa maji wa Abu Dhabi ambao umewezeshwa kwa 
kutumia vyanzo vya ndani lakini kwa namna ambayo inasaidia mji huo kuwa 
na maji ya uhakika pamoja na kwamba vyanzo vyake havifai.
Alisema
 ni matumaini yake kwamba baada ya kusikiliza mada mbalimbali wataalamu 
hao watakuwa na nafasi ya kutoa tamko la namna bora ya kushirikisha 
wadau wa maendeleo wa ndani kutengeneza miradi mikubwa ya huduma kwa 
jamii.
Pia
 alisema kwamba washiriki katika mkutano huo wa siku 2 ni pamoja na 
wadau wa maendeleo kutoka Uswisi, Sweden na Denmark wapo pia wataalamu 
wa masuala ya fedha, miradi kutoka Afrika Kusini, Ethiopia, Benin, 
Rwanda, Mali, Senegal,Uganda, Msumbiji, india, Bangladesh , Marekani na 
Tanzania.
Mkutano
 huo wa mashauriano uliandaliwa na UNCDF ikiwa ni sehemu ya utekelezaji 
wa azimio la AddisAbaba kuhusu maendeleo endelevu na umuhimu wa 
kuimarisha uwezo wa kifedha wa manispaa mbalimbali.
Mchumi Daniel Platz kutoka Umoja wa Mataifa akiwasilisha mada kwa wataalamu wa masuala ya fedha na wadau wa maendeleo waliokutana jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi
 wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa Mataifa (UNDCF), David Jackson, 
(kulia), akizungumza kwenye mkutano wa siku mbili wa wataalamu wa fedha 
na wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali Duniani, kwenye hoteli 
ya Hyaatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Februari 29, 2016. 
Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Serikali za Mitaa nchini Uganda,
 John Genda Walala

 Washiriki
 wa mkutano wa kimataifa wa siku mbili wa wataalamu wa masuala ya fedha 
na wadau wa maendeleo wakifuatilia mada ikliyorushwa kwa njia ya video 
na Profesa Paul Smoke kutoka Chuo Kikuu Cha New York, nchini Marekani.

 Mchumi, John Boex, akitoa mada kwenye ufunguzi wa mkutano huo wa siku mbili ulioanza Februari 29, 2016

 Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Serikali za Mitaa nchini Uganda, John Genda Walala, akiongoza mkutano wakati wa asubuhi

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa Mataifa (UNDCF), David Jackson, (kushoto), akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Mfuko wa Mtaji wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa(UNCDF) nchini Tanzania, Peter Malika.

Mkurugenzi
 wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa Mataifa (UNDCF), David Jackson, 
(kulia), akizungumza kwenye mkutano wa siku mbili wa wataalamu wa fedha 
na wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali Duniani, kwenye hoteli 
ya Hyaatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Februari 29, 2016. 
Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Serikali za Mitaa nchini Uganda,
 John Genda Walala


 Baadhi yawashiriki wakifuatilia kwa makini yanayoendelea katika mkutano

Mkurugenzi
 wa Maendeleo ya Fedha wa Umoja wa Mataifa (UNDCF), David Jackson, 
(kulia), akiwa kwennye mahojiano na Mjumbe kutoka nchini Uganda, Naibu 
Mkurugenzi wa usimamizi wa mikakati na maendeleo ya biashara, jiji la 
Kampala, Patrick Musoke, pembezonimwa mkutano wa siku mbili wa wa 
wataalamu wa fedha na wadau wa maendeleo 62 kutoka nchi mbalimbali 
Duniani, kwenye hoteli ya Hyaatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar es 
Salaam, Februari 29, 2016

Wajumbe wakibadilishana mawazo.(Picha zote na Khalfan Said na
Geofrey Adroph.)
 
 
 
 
 
 
 
No comments: